Chuo
Kikuu cha Nairobi kimefungwa kwa muda usiojulikana kutokana na
kinachodaiwa kuwa ukosefu wa amani katika chuo hicho kutokana na
wanafunzi kukabiliana na polisi mara kwa mara wakiandamana na hivyo
kuhatarisha usalama.
Taarifa ya seneti ya chuo hiyo imeeleza kuwa asubuhi ya leo walitoa
tangazo kwa wanafunzi wa chuo hicho kuchukua mizigo yao na kuondoka
kwenye maeneo ya chuo mpaka hapo uongozi wa chuo utakapo jiridhisha
kukifungua chuo hicho tena.Polisi waliingia chuoni walipokuwa wakikabiliana na wanafunzi waliokuwa wakiandamana kulalamikia kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kiongozi wa zamani wa wanafunzi wa chuo hicho Paul Ongili, maarufu kama Babu Owino. Owino, ambaye kwa sasa ni mbunge wa jimbo la Embakasi Mashariki jijini Nairobi, alikamatwa baada ya kudaiwa kumtukana Rais Uhuru Kenyatta.
0 comments: